Mahitaji
Njegere ½ kilo
Swaumu ½ kijiko cha chai
Beef Masala kijiko 1 cha chai
Nyanya ya Kopo vijiko 2 vya chai
Maziwa fresh kikombe 1 ½
Karoti Mbili,kata duara
Mafuta vijiko 4 vya chakula
Chumvi kwa ladha upendayo
Njia
1.Chemsha njegere adi ziive,ziwe laini na Maji yakauke.
2.Katika sufuria unga mafuta na kitunguu adi kitunguu kianze kubadilika rangi(usiache kikawa cha brown) ,Ongeza nyanya,nyanya ya kopo,chumvi,swaumu na beef masala.Kaanga adi nyanya na mafuta zitengene ndani ya sufuria.
3.Ongeza njegere na karoti ,kaanga kwa pamoja adi njegere na nyanya zishikane.Ongeza maziwa,chemsha uku unageuza mara kwa mara ili maziwa yasikatike na yasiungulie chini.Chemsha adi upate uzito unaopenda.Tayari kwa kula.
Kama familia ina watoto wadogo basi ongeza kiasi cha maziwa ili upate mchuzi mwingi.watoto wengi hupenda mchuzi wa njegere na si njegere zenyewe
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni