
Tofauti na Mtori unaopikwa kiasili,mtori huu wa nazi nimeupa vionjo mbalimbali ili kupata ladha mpya na virutubisho vingi.
Mahitaji
- Ndizi mbichi 5 (tumia ndizi bukoba)
- Nyama ya ng’ombe ½ Kilo
- Vitunguu maji 2
- Karoti kubwa 1
- Nazi 1 (Nazi ya azam au nazi yaunga)
- Blue banda kijiko 1 cha chai
- Chumvi kwa ladha upendayo
Si lazima kutumia vipimo hivi,kua huru kukadiria vipimo kutokana na kiasi cha mtori unaotaka kupika.
Njia1.chemsha nyama adi ikaribie kuiva ,iwe na supu nyingi.
2.Katika sufuria lingine,weka ndizi ,vitunguu na karoti.kisha mimina nyama juu yake na supu yote.chemsha adi ndizi ziive nakua laini,pia zibaki na supu kiasi
- Pika ndizi kwenye moto wa wastani ili ziive nakulainika haraka,moto mkali utaunguza ndizi na hazitaiva haraka
- Kama supu ya nyama nikidogo ongeza maji kiasi ili kuivisha ndizi na nyama
4.katika jagi lakusaigia matunda (blender) weka ndizi na supu yake kisha ongeza nazi na usage kwa pamoja adi uwe mtori laini
- Badala yakusaga mtori kwenye blender unaweza kupika kiasili kwa kupekecha mtori kwa kutumia pekecho kama unalo.
- Mtori ukiwa mzito sana ongeza supu iliyobaki au maji adi kupata uzito upendao
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni